Monday, November 3, 2014

Nyimbo Za Kikristo: 201-220

201. Hunipenda Pia.
He Loves me, too

1. Mungu huona videge wanaoanguka;
Akiwapenda videge,vile hunipenda.

Hunipenda, hunipenda, pia;
Najua ananipenda niliye mdogo.

2. Rangi ya namna nzuri upamba maua;
Akiyapenda maua, vile unipenda.

3. Mungu aliyeviumba videge, maua,
Atasahau watoto kweli huwapenda.

202. Sikia Mlio
Hear the Pennies Dropping

1. Sikia mlio! Pesa koponi
Zinalialia—zote kwa Yesu.

Kuanguka kuanguka pesa koponi,
Kila moja kwako, Yesu zipokee.

2. Huanguka pesa toka mikononi:
Sadaka kwa Yesu ya kundi dogo.

3. Tulio wadogo tuna haba tu;
Tuishapo kuwa Pendo 'tazidi.

4. Wenye mali chache tumpe moyo;
Kwa furaha tupu atakubali.

203. Ya Saba Ni Kwa Yesu
The Seventh Day Is For Jesus

1. Siku sita fanya kazi, Ya saba ni kwa Yesu.
Hapo tunapo pumzika, kwani ni yake Yesu.

Moja, mbili, tatu,nne, tano, sita, zote kwetu;
Lakini tutakumbuka, Ya saba ni kwa Yesu.

2. Huonyesha ya kufanya, Kwa kuwa ni ya Yesu,
Na atuonyesha njia, tutamfuata Yesu.

3. Tuombe kila Sabato, Na kujifunza kwake;
Tutamtii daima, tutakaa na Yesu.






204. Kuwa Na Yesu Nyumbani
Happy, Happy, Home

1. Kuwa na Yesu nyumbani,
Furaha nyingi,
Furaha nyingi, Furaha nyingi.
Kuwa na Yesu nyumbani,

2. Yesu yu ndani ya Baba,
Nyumba salama, nyumba salama, nyumba salama;
Yesu yu ndani ya Baba.
Nyumba salama, nyumba salama.

3. Yesu yu ndani ya Mama . . .

4. Yesu ndani ya watoto . . . .

205. Msifu Mungu Ee Watoto
Praise Him, Praise Him

1. Msifu Mungu, Ee watoto wote,
Yu pendo, Yu pendo;
Msifu, Msifu, Ee watoto wote
Mungu ni upendo.

2. Tunampenda, Ee watoto wote,
Yu pendo, Yu pendo,
Tunampenda, Ee watoto wote
Mungu ni upendo.

3. Timikeni, Ee watoto wote.
Yu pendo, Yu pendo,
Tumikeni, Ee watoto wote
Mungu ni upendo.

206. Mwokozi Wangu Anipenda
Now I Belong To Jesus

1. Mwokozi wangu alinipenda,
Maovu ayanitengi naye,
Alijitoa, kuniponya,
Sasa mimi wake.

Mimi wake kabisa,
Naye Yesu wangu,
Si kwa wakati huu tu,
Bali na milele.

2. Dhambi nilijidhili sana,
Yesu akaja kunikomboa,
Akanitoa sumbukoni,
Sasa mimi wake.

3. Furaha nyingi moyoni mwangu,
Bwana Yesu kunifanya huru,
Kunitwaa kwa damu yake,
Sasa mimi wake.

207. Nani Afanya Maua
Who Makes The Flowers

1. Nani ayafanya maua, maua,
Nani ayafanya—Mungu juu.

2. Nani apambaye machweo, machweo,
Nani ayapamba—Ni Mungu.

3. Nani afanya theluji, theluji,
Nani aifanya—ni Mungu.

208. Mungu Afanya Upinde
The Rainbow

1. Nani afanya upindi,
Namjua, namjua
Mungu afanya upindi
Nampenda kwa hiyo.

2. Mungu atuma upindi
Ni bora mweupe,
Mungu atuma upindi,
Kwamba yu karibu.

209. Napenda Sana Kifika
I Love to Come to Sabbath School

1. Napenda sana kufika, skuli ya Sabato
Napenda sana kufika, siku ya Sabato

2. Napenda sana kuimba, habari za Yesu,
Napenda sana kuimba, siku ya Sabato.

3. Napenda sana kutoa, sadaka kwa Yesu,
Napenda sana kutoa, siku ya Sabato.

4. Napenda sana kuomba kwa Yesu, kwa Yesu,
Napenda sana kuomba, siku ya Sabato.

5. Napenda sana kujua, maneno ya Yesu,
Napenda sana kujua, siku ya Sabato.

6. Napenda sana kusema, Fungu la kukariri,
Napenda sana kusema, Siku ya Sabato.

210. MAITIKIO
Roho Wa Mungu Wangu
Spirit of the Living God

Roho wa Mungu wangu, Nakuhitaji!
Roho wa Mungu wangu, Nakuhitaji!
Unilinde na unijaze;
Roho wa Mungu wangu, Nakuhitaji!

211. Moyoni
(Into My Heart)

Moyoni, moyoni; Ingia moyoni, Yesu.
Njoo leo, njoo kukaa, Ingia moyoni Bwana.
Moyoni, moyoni, Angaza moyoni Yesu,
Ng'aa leo siku zote, Angaza moyoni Bwana.

212. Mtazame Mwokozi
(Turn Your Eyes Upon Jesus)

Mtazame Mwokozi,
Usoni Mwake mzuri,
Mambo ya dunia hugeuka,
Usowake tukiuona.

213. Niwe Nao Uzuri Wa Mwokozi
(Let the Beauty of Jesus)

Niwe nao uzuri wa Mwokozi,
Nazo huruma Zake na usafi,
Roho Mtakatifu anibadilishe,
Aonekane Yesu ndani yangu.

214. Nataka Niwe Tayari
(I Want to be Ready When Jesus Comes)

Nataka niwe tayari, Bwana,
Nataka niwe tayari, Bwana,
Furaha za ulimwengu ni bure;
Nilinde hata uje!

215. Ulimwengu Wataka
(What the World Needs is Jesus)

Ulimwengu wataka kumwona Yesu;
Ulimwengu wataka kumwona Yesu.
Analeta furaha, shangilio kutosha,
Ulimwengu wataka kumwona Yesu.

216. Moyoni 'Nijaze
(With Thy Spirit Fill Me)

Moyoni 'nijaze,
Na Roho wa Yesu;
Nataka kujitoa,
Moyoni 'nijaze.

217. Omba Sana Asubuhi
(Whisper a Prayer in the Morning)

Omba sana asubuhi,
Omba sana mchana,
Omba sana na jioni,
Bwana hutusikia.

Mungu hujibu maombi,
Asubuhi na mchana,
Hata hutungojea tena,
Wakati wa jioni.

Na tuimbe asubuhi.
Tena saa za mchana.
Hivi tutafurahi Naye.
Pumziko la jioni.

218. Yesu Mwokozi Mpendwa
(Wonderful, Wonderful Jesus)

Yesu Mwokozi Mpendwa.
Hakuna mwingine!
Yesu Mwokozi Mpendwa,
Yesu Mwokozi Mpendwa,
Nakutazama wewe pekee,
Yesu Mwokozi Mpendwa,
Ninakutafuta;
Wewe u mali yangu.
Sasa na milele.

219. Pambazuka Nuru
(There's a New Day Dawning)

Pambazuka nuru,
Siku mpya yaja,
Basi amkeni na kuimba,
Ninyi nyote!
Pambazuka nuru,
Siku mpya yaja,
Yesu atakaporudi kama Mfalme!

220. Kwa Heri
(Goodbye Chorus)

Kwa heri, Mungu awalinde;
Kwa heri, na awaongoze;
Kwa heri, na kuwapa amani,
Bwana awabariki.

2 comments:

  1. May You be blessed brother. Thank you for the good work. Found that 181-200 is missing and my favourite is no 181-Mahali Pa Maji Mazuri. Kindly add them.

    ReplyDelete