Monday, November 3, 2014

Nyimbo Za Kikristo: 101-120

101. Yesu Akwita
Jesus Is Tenderly Calling Today

1. Yesu akwita, akwita wewe, Uje leo, uje leo,
Kwani kusita, akwita wewe Unatanga upeo;

Msikie, msikie,
Yesu akwita, ujitoe moyo sasa.

2. Wliochoka, na wapumzike, Uje leo, uje leo,
Wenye mizigo, wenye huzuni Wapate mapumziko.

3. Anakungoja uliye yote, Uje leo, Uje leo,
Uliyekosa, usijifiche: Woshwe, uvikwe nguo.

4. Yesu asihi wakawiao, Waje leo, waje leo,
Watafurahi waaminio; Amka, upesi, Njoo.

102. Mlango Pa Moyo
There's a Stranger as the Door

1. Mlangoni pa moyo; Mgeni! (Amesimama)
Amesimama pale, Mgeni! (Amesimama)
Umkaribishe sasa,
Umkaribishe Mwana
Wa Baba wa upendo: Mgeni! (Umkaribishe)

2. Moyo wako kwa Bwana, Fungua. (Fungulieni)
Asikuache mbali, Fungua. (Fungulieni)
Umkubali Rafiki,
Roho atafariji
Naye atakutunza: Fungua. (Fungukieni)

3. Usikie sauti Ya Bwana. (Uisikie)
Uyachague mambo Ya Bwana. (Mambo ya Bwana)
Ufungue mlango,
Usimwambie bado:
Jina lake tumai---- Yu Bwana. (Jina la Bwana)

4. Na ufungue moyo, Kwa Bwana (Fungulieni)
Utapewa msaada, Wa Bwana (Msaada wetu)
Uzuri utavikwa
Dhambi ataondoa,
Ukifungua moyo. Kwa Bwana (Fungulieni)





103. Njoni Kwangu
Softly and Tenderly

1. Yesu huita kwa upole mwingi, atwita wewe nami;
Moyoni mwetu hungoja, hukesha, Hukungojea wewe.

"Njoni kwangu, Mliochoka, njoni:
Yesu huita kwa upole mwingi, Akwita, "uje kwangu"

2. Atuombeapo usikawie, Hutuombea sisi;
Usidharau wema ma huruma, Huruma kwetu sisi.

3. Siku za maisha hupota hima, Hupita kwako, kwangu;
Usiku waja, kifo kinakuja, Huja kwako na kwangu.

4. Fikiri juu ya upendo wake, Upendo kwako, kwangu;
Dhambi zetu amekwisha samehe. Masamaha ni yetu.














104. Yesu Aliniita "Njoo"
I Heard the Voice of Jesus Say

1. Yesu aliniita, "Njoo Raha iko kwangu,
Kichwha chko ukilaze Kifuani mwangu"
Nilikwenda kwake mara, sana nilichoka;
Nikapata kwake raha Na furaha tena.

2. Yesu aliniita, "Njoo, Kwangu kuna maji;
Maji ya Uzima, bure, Unywe uwe hai."
Nilikwenda kwake mara na maji nikanywa;
Naishi kwake na kiu Kamwe sina tena.

3. Yesu aliniita, "Njoo, Dunia i giza,
Ukinitazama, nuru Takung'arizia.'
Nili kwenda kwake mara, Yeye jua langu,
Ni kila wakati mwanga Safarini Mwangu.














105. Mchungaji Mpenzi
Lovingly, Tenderly Calling

1. Mchungaji mpenzi hukuita uje
Katika zizi lake Panapo salama;
Akina wanawake, waume vijana,
Yesu aliye kweli, huwaita kwake

Huita kwa moyo wa huruma, 'Uluyepotea uje kwangu';
Hivi kukungoja anadumu Bwana Yesu Mchunga.

2. Akatoa maisha kwa ajili yetu;
Ataka wapotevu waje kwake sasa;
Tusijihatirishe; Kwake tu salama;
Sikia wito wake, Mchungaji wetu.

3. Tusikawie tena, adui shetani,
Kama Mbwa wa mwitu, atatuharibu;
Tunaitwa na Yesu, Mkombozi wetu,
Tuingie zizini, panapo nafasi.











106. Huna Kitu Kwa Yesu?
Nothing for Jesus

1. Ukitafuta mali, Huna wasaa kwa Yesu?
Kwa matendo ya haki Huna wasaa kwa Yesu?
Ansa za kunia, Mambo yako ya raha
Haya unatafuta; Huna wasaa kwa yesu?

2. Mambo yanakusonga: Kwake huna nafasi?
Watekwa na dunia, Kwake huna nafasi?
Humwani m-langoni, Anapopiga hodi?
Daima hukusihi: Kwake huna nafasi?

3. Sa-a ni za thamani, Kwake huna nafasi?
Wala hamfnyi bidii, Kwake hamnayo kazi?
Hamkufika kwao Waliomo shimoni
Na waliopotea? Kwake hamnayo kazi?

4. Na wazaa majani tu? Huna tunda kwa Yesu?
Mikono i mitupu, Huna tunda kwa Yesu?
Huna chembe kwa ghala kazi yako kulipa;
Wala huna furaha Unapomwona Yesu?










107. Nipo Bwana, Nitume
Hark! The Voice Of Jesus

1. Sauti ni yake Bwana, "Kwenda, nani tayari"
Mavuno yanakawia, Nani atayavuna?
Kwa kudumu amaita, Zawadi atatoa;
Nani atakayejibu "Nipo Bwana, nitume."

2. Kana huwezi safari Hata Nchi za mbali,
Pana watu karibuni Wasio mjua Yesu;
Kama huwezi kusema Jinsi ya malaika,
Waweza kuutangaza Upendo wa mwokozi.

3. Ingawa huwezi kuwa Mkesha mlangoni,
Ukiwatolea watu Nafasi ya uzima;
Kwa sala na kwa sadaka Watoa msaada,
Kama Harun mwaminifu, Kuinua Mikono.

4. Roho za watu zikifa, Bwana akikuita,
Usiseme kwa uvivu, "Hakuna kazi kwangu."
Kwa furaha anza kazi Ile akiyokupa,
Ukajibu mara moja "nipo Bwana, nitume."









108. Tumesikia Mbiu
We Have Heard a Joyful Sound


1. Tumesikia mbiu: Yesu huokoa;
Utangazeni kote, Yesu Huokoa.
Tiini amri hiyo: nchimi baharini,
Enezeni mbiu hii: Yesu huokoa.

2. Imba nawe askari: Yesu huokoa;
Kwa nguvu ya kombozi, Yesu huokoa;
Imbeni wenye shida, unapounwa moyo,
Na kaburini imba: Yesu huokoa.

3. Mawimbini uenee. Yesu huokoa.
Wenye dhambi jueni: Yesu huokoa;
Visiwa na viimbe, vilindi itikeni,
Na nchi shangilie: Yesu huokoa.

4. Upepo utangaze: Yesu huokoa.
Mataifa ya shangaa: Yesu huokoa;
Milimani, bondeni, sauti isikike
Ya winbo wa washindi: Yesu huokoa.








109. Anisikiaye
Whoever heareth

1. Anisikiaye, aliye yote, sana litangae, wajue wote,
Duniani kote neno wapate, atakye na aje!

Ni "atakaye," Ni "atakaye";
Pwani hata bara, na litangae:
Ni Baba mpenzi alinganaye atakaye na aje.

2. Anijiliaye, Yesu asema, asikawe, aje hima mapema
Ndimi Njia, kweli, ndimi uzima: atakaye na aje!

3. Atakaye aje, ndiyo ahadi; atakaye hiyo haitarudi!
Atakaye lake, ni la ahadi! Atakaye na aje.

110. Mlango Wazi
There is a Gate

1. Mlango uko wa wema, Mlango wazi huo:
Yesu aneufungua Na hakuna kufunga.

Mlango wazi, ajabu, Uliachwa wazi kwangu?
Kwangu, Kwangu? Wazi, wazi kwangu?

2. Mlango hukaa wazi watu waokolewe:
Maskini ma matajiri Wa mataifa yote.

3. Maadanu mlango wazi, Rafiki kaza mwendo;
Msalaba ukubali- Amana ya upendo.

4. Msalaba tutabeba Daima, na furaha!
'pendo la Yesu hushinda. Unainama kwake!















111. Tabibu Mkuu
The Great Physician

1. Tabibu mku-u huyu, Yesu mwenye huruma:
Atuletaye faraja : Yesu mwokozi wetu.

Imbeni, Malaika Sifa za bwana wetu;
Jina la pekee kwetu, ni la Yesu Bwana.

2. Mwana kondo-o msifuni Mwokozi:
Hatia zote na dhambi Huziondoa Yesu.

3. Hakuna jina jingine Linalofa-a sifa:
A-u kutufurahisha, Isipo kuwa lake.

4. Naye atakapokuja Na utukufu wake,
Tutafurahi milele kuka-a kwake Bwana.


112. Wewe Umechoka Sana?

1. Wewe umechoka sana? Wataka raha?
Kwake Yesu utapata –Msaada.

2. Alama anazo Yeye? Sana! Makovu
Ya mikono, na miguu, Na mbavu.

3. Naye amevikwa taji Kichwani mwake?
Taji, kweli, alivikwa –Miiba!

4. Huku nikimfuata, Nipate nini?
Maonjo nje, na ndani—Amani.

5. Kwamba namwandama Yeye, Mwisho ni nini?
Kurithi futaha naye---Milele.

113. Bubujiko
There Is a Fountain

1. Damu imebubujika, Ni ya Imanweli,
Wakioga wenye taka, Husafiwa kweli.

2. Ilimpa kushukuru Mwivi mautini;
Nami nisiye udhuru, Yanisafi ndani.

3. Kondo-o wa kuuawa, Damu ina nguvu,
Wako wote kuokoa kwa utimilivu.

4. Bwana, tangu damu yako Kunisafi kale,
Nimeimba sifa zako. 'taimba milele.

5. Bwana, umenikirimu Nisiyestahili
Kwa damu yako, sehemu Ya mali ya kweli.

6. Nikubali kumwimbia Mbinguni milele.
Mungu nitamsifia Jina lako pweke.

114. Yesu Nataka Kutakaswa Sana
Lord Jesus, I Long to be Perfectly Whole

1.Yesu Mwokozi Ili nitakaswe, nataka mouo uwe enzi Yako.
Ukiagnushe kilichoinuka unioshe sasa niwe mweupe.

Mweupe tu, ndiyo mweupe,
Ukiniosha nitakuwa safi.

2. Bwana Yesu sasa unitazame, unifanye niwe dhabihu hai."
Najitoa kwako, na moyo, vyote; unioshe sana niwe mweupe.

3.Bwana kwa hiyo nakuomba sana, nakuongojea miguuni pako,
Wanaokuja hutupi kamwe, unioshe sasa niwe mweupe.

115. Naendea Msalaba
I am Coming To The Cross

1. Naendea msalaba, Ni mnyonge, mpofu,
Yapitayo naacha nipe msalaba tu.

Nakutumaini tu, wee Mwana wa Mungu;
Nainamia kwako; Niponye sasa, Bwana.

1. Nakulilia sana: Nalemewa na dhambi;
Pole Yesu asema: "Nitazifuta zote."

3. Natoa vyote kwako, nafasi nazo nguvu,
Roho yangu na mwili viwe vyako milele.

4. Kwa damu yake sasa amenivuta sana,
Upendo hubidisha, nimtafute Mwokozi.
116. Moyo Safi
One Thing I of the Lord Desire

1. Bwana ninataka hili, kwa kuwa nimechafuka,
Kwa moto au kwa maji unisafishe kabisa.

Unisafishe Mwokozi ndani, na nje, kwa moto—
Utakavyo: ili dhambi ife kwangu, ife kwangu.

2. Kupewa hekima yote, itakuwa tunu kubwa;
Lakini moyo safi ni, bora kwangu, bora kwangu!

3. Mpaka moyo ni safi siwezi kuyafahamu
Mambo mazuri ya mbingu, mambo mazuri ya mbingu.

117. Wamwendea Yesu
Have You Been to Jesus?

1.Wamwendea Yesu kwa kusafiwa. Kuoshwa kwa damu ya kondoo?
Je, neema yake yatumwagiwa? Waoshwa kwa damu ya Kondoo?

Kuoshwa, kwa damu Itutakasayo ya Kondoo?
Ziwe safi nguo nyeupe sana; waoshwa kwa damu ya Kondoo.

2.Wamwandana daima Mkombozi.Waoshwa kwa damu ya Kondoo?
Yako kwa Msulubiwa mavazi? Waoshwa kwa. Damu ya Kondoo?

3.Atakapokuja Bwana-arusi Uwe safi katika damu!
Yafae kwenda Mbinguni mavazi: Yaoshwa kwa damu ya kondoo?

4.Yatupwe Yalipo na takataka; Uoshawe kwa damu ya Kondoo:
Huoni kijito chatiririka Uoshwe kwa damu ya Kondoo?


118. Nilipotoka Kabisa
I've Wandered Far Away

1.Nilipotoka kabisa, sasa narudi
Nikakawia dhambini, Bwana narudi.

Narudi nyumbani: daima kwako.
Kwa upendo nipokee: Naja nyumbani.

2.Nikasusurika sana, sasa narudi
Mwenye uchungu natubu, Bwana narudi.

3.Nimechoka maovuni, sasa narudi;
Pendo lako lanivuta, Bwana narudi.

4. Ndilo tumaini langu, sasa narudi;
Yesu alinifilia, Bwana narudi.

5. Damu yake yanitosha, sasa narudi;
Unioshe kenyekenye, bwana narudi.

119. Alilipa Bei
I Hear the saviour Say

1.Yesu anasema, "Wewe huna nguvu
Kesha ukaombe, Na uje, Mwanangu.

Alilipa bei, Nawiwa naye;
Dhambi ilitia waa, aliiondoa.

2. Bwana, nimeona Uwezo wako tu
Waweza 'takasa Mioyo michafu.

3. Sina kitu chema Kudai Neema,
Hivi nitafua Mavazi kwa damu.

4. Ninaposimama Juu ya mawingu,
Taji nitaweka Miguuni pa Yesu.


120. Msalaba wa Yesu
Jesus, Keep Me Near The Cross

1. Msalaba wa Yesu, Nikae karibu;
Pale pana chemchemi Ya kuponya dhambi.

Pale msalaba Msalaba wake,
Huo ni sifa yangu Kwa maisha yote.

2. karibu msalaba Nalitetemeka,
Pendo likaniona Likanirenemu.

3. Unikumbushe yesu, Nikuone pale;
Niupate upendo Na kuvutwa nao.

4. Karibu msalaba, Kwa kutegimea,
Kukesha na kungoja, Nitakaa pale.

5 comments: