Monday, November 3, 2014

Nyimbo Za Kikristo: 161-180

161. Piga Panda
Lift Up The Trumpet

1. Piga panda na ya makelele; Yesu yuaja tena!
Ipate sauti, imba sana; Yesu yuaja tena!

Anakuja, anakuja; Yesu yuaja tena!

2. Itoe mwangi sana vilima; Yesu yuaja tena!
Yuaja kwa utukufu mwingi, Yesu yuaja tena!

3. Itangazwe mahali po pote; Yesu yuaja tena!
Mwokozi aliye tufilia, Yesu yuaja tena!

4. Kuona machafuko twajua Yesu yuaja tena!
Mataifa ya kasiriana, Yesu yuaja tena!

5. Maradhi, hofu hutuhubiri Yesu yuaja tena!
Taabu, njaa hutulilia Yesu yuaja tena!

162. Tumaini Liko
There Is a Blessed Hope

1. Tumaini liko La thamani kuu,
Kupita anasa tupu zake ulimwengu.

2. Pana nyota nzuri: Nuru itoayo
Kwetu wakati wa kifo Ndio ufufuo.

3. Zikiumwa roho Na hofu, mashaka,
Sauti hutuambia Mungu hutupenda.

4. Kutoka Kalwari Sauti hunena;
Nyota ni nuru ya mbingu, Tumaini letu.

















163. Anakuja, Bwana Yesu
It May Be A Morn

1. Pengine ni saa ya kupambazuka, Mishale ya jua ipenyapo giza,
Kwamba atakuja Yesu mtukufu, Awapokee wake.

Bwana itakuwa lini Tutapoimba
"Anakuja, Bwana Yesu, Aleluya, Amin, Aleluya, Amin?"

2. Pengine mchana, pengine jioni, Pengine usiku wa manane, giza
Itatoweka kwa fahari akija, Awapokee wake.

3. Majeshi yake yataimba "Hosana," Na watakatifu waliotukuzwa
Watamsifu kwa kuwa amekuja Awapokee wake.

4. Furaha tukiitwa pasipo kufa, Pasipo kuona maradhi, machozi;
Kuchukuliwa winguni kwa fahari Akija kwa watu wake.

164. Mishale Ya Nuru
The Golden Mornig

1. Unakaribia wakati wa Kuja kwa Yesu.
Atawachukua watu wake Nyumbani juu.

Tunaiona mishale ya nuru Inayopenya giza;
Tunaiona mishale ya nuru Ya ufunuo.

2. Injili inatangazwa pote kwa mataifa;
Bwana wa Arusi atakuja Na tarumbeta.

3. Pamoja na malaika zake Bwana arudi,
Awapeleke waaminifu Wasife tena.

4. Wapenzi waliotengwa kale Watakutana;
Machozi yao wenye huzuni Yatafutika.

165. "Uwe Imara"
Sweet Promise Is Given

1. Ahadi tamu kwa waamini, Tazama nakuja upesi sana.
Uwe imara, hatari kubwa: Ndugu usilale, bali ukeshe.

Uihifadhi imani yako,--Dunia mpya itatolewa
Njoo ingia furaha yangu; Taji zinangoja; Uwe imara.

2. Tatakesha na kutoa sala; Atakuja kama mwivi kwa wengi;
Ya kwamba yu karibu twajua, Ila hatujui ni siku gani.

3. Tunategemea Neno lake, Ambalo latangaza kuja kwake,
Tumaini letu ni ahadi: "naja karibuni, uwe imara."

166. Furaha Kwa Ulimwengu
Joy to the World
1. Furaha kwa ulimwengu, Bwana atakuja!
Kila moyo umpokee, Viumbe imbeni,
Viumbe imbeni, Viumbe vyote imbeni.

2. Na Bwana atatawala: Watu na waimbe;
Mit, milima na mawe Kariri furaha,
Kariri furaha, Kariri furaha kubwa.

3. Atatawala kwa wema; Atawafundisha
Mataifa haki yake, Ajabu za pendo,
Ajabu za pendo, Ajabu za pendo lake.

167. Yu Hai, Yu Hai
(He Lives, He Lives)

1. Yesu Bwana Mwokozi aishi milele,
Najua kwamba Yupo pamoja na mimi;
Sauti nasikia, Rehema naona;
Wakati namhitaji, yupo nami.

Yu hai, Yu hai,Yu hai Bwana Yesu!
Atembea, azungumza nami siku zote.
Yu hai, Yu hai, kutoa uzima!
Hivi ndivyo nijuavyo,
Yu hai ndani yangu!

2. Ulinzi Wake upo naona dhahiri,
Miguu ichokapo, sikati tamaa.
Najua an'ongoza kupota dhoruba,
Siku ya kuja kwake nitamwona.

168. Tarumbeta Ya Mwana
Wahen the Trumpet of the Lord

1. Tarumbeta ya mwana itakapolia mara,
Milele itakapopambazuka,
Nao wa haki watakapokusanyika ng'ambo,
Majina yaitwapo, lo!—niweko.

Majina yaitwapo, lo!—
Majina yaitwapo, lo!—
Majina yaitwapo, lo!—
Majina yaitwapo, lo!—niweko.

2. Siku ile watakatifu watakapoamka
Na kuondoka huru kaburini
Watakapokusanyika makaoni kule juu,
Majina yaitwapo, lo—niweko.

3. Tutende kazi kwa yesu mchana kutwa kwa bidii,
Tutangaze kote pendo lake kuu,
Nayo kazi itakapotimika hap chini
Majina yaitwapo, lo—niweko.

169. Tutashindae Hukumuni?
When Jesus Shall Gather

1. Hapo Yesu atakapoita mataifa mbele yake,
Tutashindaje kwenye hukumu mbele ya kiti cha enzi?

Atakusanya ngano ghalani, atatupambali makapo;
Tutashindaje hukumuni siku kuu ya kiyama?

2. Je, tutasikua neno tamu: "vema, wewe mtumwa mwema,"
Ama wenye uchunguna hofu tutakatazwa ufalme?

3. Atakubali tu kwa furaha watoto wake wapendwa,
Atawapa mavazi meupe, wakea tayari kumlaki.

4. Hivyo tukeshe, nasi tungoje, wenye taa zinazo waka;
Tutakapoitwa arusini tuwe tayari kumlaki.

5. Roho ikielekea mbingu twangoja wenye saburi,
Hata safari yetu iishe, tukae kwake milele.

170. Jina Langu Limeandikwa Je?
Lord, I Care not for Riches

1. Siitafuti mali, wala utajiri;
Nataka kwa yakini nipate Mwokozi.
Chuoni mwa Ufalme, niambie Yesu,
Jina langu yakini limeandikwa, Je?

Limeandikwa, Je? Jina langu huko?
Kitabuni mbinguni, limeandikwa je?

2. Dhambi zangu ni nyingi, ni kama mchanga,
Lakini damu yako, Mwokozi, Yatosha;
Kwani umeahidi: zijapo nyekundu
Zitakuwa nyeupe ilivyo theluji.

3. Mji mzuri sana, wa majumba makuu,
Walipo malaika, mji bila ovu;
Wakakapo walio na mavazi safi,
Limeandikwa sasa, jina langu huko?

171. Hukumu
The Judgment Has Set

1. Imeanzishwa hukumu mbinguni; Tutasimamaje pale
Apomapo Mungu hakimu kula wazo na tendo?

Tutasimamaje sote katika siku kuu ile?
Dhambi zitu zitafutika ama zitatuangusha?

2. Wametangulia wafu kupimwa, Kitambo ndipo wahai,
Watapokea neno la mwisho, Vitabuni mwa Mungu.

3. Tutasimamaje usiku ule, Siri zetu, kila moja,
Zafunuliwa toka vitabu; Yesu atusaidie!

172. Mfalme Ajapo
Called To The Feast

1. Mfalme wetu atuita tukae karamuni kwake;
Itakuwaje nasi kule Bwana akija?

Bwana ajapo, ndugu, Bwana ajapo!
Itakuwaje na sisi, Bwana akija?

2. Atavikwa vizuri sana,taji badala ya miiba;
Kweli tokeo la fahari Bwana ajapo.

3. Kwa fufaha awakubali wenye mavazi ya arusi;
Tu wa heri tukimridhisha Bwana ajapo.

4. Kutakuwako na utengo: watalia waliomwasi;
Cha kutisha kitambo kile Kristo ajapo!

5. Mfalme utupe neema sisi tunapokungojea
Tusiogope kukuona ujapo Bwana.
173. Hatujui Saa
We Know Not the Hour

1. Hatujui sa-a ya kuja kwwa Bwana, Lakini dakiki zasema karibu
Atakporudi,--lakini kwa kweli Hatujui sa-a.

Atakuja, kwa vile tukeshe;
Atakuja Mwokozi, Aleluya!
Atakuja kwa fahari yu Baba yake,--
Hatujui sa-a.

2. Pana nuru kwao wapendao haki, pana kweli katika chuo cha Mungu;
Unabii hufundisha kuja kwake,--Hatujui saa.

3. Tutakesha na tutaomba daima, Tutafanya kazi mpaka akija,
Tutaimba na tutasoma ishara,--Hatujui saa.

174. Tukimngojea
We Know not the Time when He Cometh

1. Sijui atakapokuja, 2. Nakumbuka huruma zake,
Mchana au usiku; Bei ya wokovu wetu:
Labda sa-a ya alasiri, Aliacha nyumba tukufu
Pengine ni alfajiri. Awafilie wabaya.
Hutwambia tuwe tayari, Ninadhani itampendeza,
Ta-a zetu tusizime; Kama sisi watu wake,
Ili ajapo atukute; Tukionyesha pendo letu,
Tuwe tukimngoja Yeye. Tuwe tukimngoja Yeye

Tu - - - kimngojea - - - a, 3. Ee Yesu, Mwokozi mpendwa,
(kukesha, tunakungoja Wewe) Wajua nalihifadhi
Tu - - - kimngojea - - - a, Tumaini la kukuona.
(kukesha, tunakungoja Wewe) La kukaribishwa nawe
Tu - - - kimngojea - - - a, Ukija kwa watu wengine,
(kukesha, tunakungoja Wewe) Kama mhukumu wao,
Twakesha, twamngoja Yeye. Kwangu utakuwa rafiki,--

Nakesha, nakungojea.

175. Uso Kwa Uso
Face to Face

1. Nitaonana na Yesu, uso kwa uso kweli;
Siku ile shangwe tele nitamwona Mwokozi.

Tutaonana kwa macho, huko kwetu mbinguni;
Na kwa utukufu wake, nitamwona milele.

2. Sasa siwezi kujua jinso alivyo hasa,
Bali atakapokuja, nitamwona halisi.

3. Mbele yake yafukuzwa machozi na huzuni;
Kipotovu kitanyoshwa, fumbo litafumbuka.

4. Uso kwa uso! Hakika palepale furaha;
Nitafurahi kabisa nikimwona Mwokozi.

176. Ati Tuonane Mtoni?
Shall we Gather at River

1. Ati twonane mtoni? maji mazuri ya mbingu;
Yanatokea mwangani, penye kiti cha Mungu.

Naam, twonane mtoni! Watakatifu, kwenu ni mtoni!
Tutakutanika kule mtoni penye kiti cha Mungu.

2. Tukitembea mtoni na Yesu mchunga wetu,
Daima tu ibadani usoni pake kwetu.

3. Tukisafiri mtoni tutue ulemeao,
Wema wa Mungu yakini: una taji na vao!

4. Kwang'ara sana mtoni cha Mwokozi ni kioo,
Milele hatuachani tumsifu kwa nyimbo.

5. Karibu sana mtoni, karibu tuatawasili,
Mara huwa furahani na amani ya kweli.

177. Kazi Yangu Ikiisha
When my Life-work is Ended

1. Kazi yangu ikisha, nami, nakiokoka,
Na kuvaa kutokuharibika,
Nitamjua Mwokozi; nivukapo ng'amboni
Atakuwa wa kwanza kunilaki.

Nitamjua, nitamjua,
Nikimwona uso kwa uso;
Nitamjua, nitamjua,
Kwa alama za misumari.

2. Kuona uso wake utanipa furaha,
Furaha isiyo ya kukomesha;
Nitamsifu Mwokozi kwa rehema na pendo
Vilivyo nipa pahali mbingini.

3. Nao walio kufa katika Bwana Yesu,
Nitawaona tena huko juu;
Lakini nifikapo kwake huko mbinguni,
Nataka kumwona Mwokozi kwanza.

4. Milangoni mwa mji Bwana atanipisha,
Pasipo machozi awla huzuni.
Nitauimba wimbo wa milele: lakini
Nataka kumwona Mwokozi kwanza.




178. Ukingoni Mwa Yordani
On Jordan's Stormy Banks

1. Ukingoni mwa Yordani ninaangalia
Bara nzuri ya Kaanani, ninayotamani.

Tutakaa pamoja na Yesu,
Katika pwani yenye raha;
Tutaimba wimbo wa Musa na Kondoo,
Milele hata milele.

2. Bara ile ina nuru, nuru ya milele;
Kristo, Jua, hutawala, hufukuza giza.

3. Nitapafikia lini na kubarikiwa,
Penye ufalme wa Baba. Na kumwona uso?

4. Furaha yangu rohoni ni kuchukuliwa;
Siyaogopi mawimbi katika Yordani.

179. Watafurahi
O There'll Be Joy

1. Wavunaji watafurahi, pale watakapo rudi,
Wakiyaleta mavuno hata Yerusalemu.

Furaha wataipata, furaha hata milele,
Furaha, wataipata, wakati wa mavuno.

2. Na siku ile tutaimba, kumshukuru na kumsifu
Bwana Yesu Jumbe wetu, kule Yerusalemu.

3. Wavunaji watafurahi makaoni mwa milele
Yaliyowekwa tayari kule Yerusalemi.

180. Pana Mahali Pazuri Mno
There's a Land

1. Pana mahali pazuri mno,
Twapaona kwa mbali sasa;
Baba yetu angoja pale,
Amepanga makao yetu.

Kitambo tu bado,
Tutakutana ng'ambo pale.
Kitambo tu bado,
Tutakutana ng'ambo pale.

2. Tutaimba pale kwa moyo
Nyimbo tamu za wenye heri.
Na rohoni hatutaona
Tena haja ya kupumzika.

3. Kwa Baba yetu mkarimu
Tutatoa shukrani sana,
Kwa kipaji cha pendo lake
Na baraka anazotupa.

12 comments: